Kuzaliwa Imam Redha (AS)

Imamu Ali Ar-Ridha (a.s.) alizaliwa mnamo tarehe 11 ya mwezi wa Dhul-Qa'adah (Mfunguo Pili) wa mwaka wa 148 Hijiriya, mjini Madina. Wakati huo baba yake Imamu Jaafar As-Sadiq (a.s.) alikuwa keshafariki mwezi mmoja uliopita, kwenye tarehe 15 ya mwezi wa Shawwal (Mfunguo Mosi) na kuzaliwa kwa mtoto huyu kulileta faraja kwa jamii hii iliyoondokewa na baba yao.
JINA NA NASABA YAKE
Jina lake lilikuwa Ali "Kun'yat" (jina la utoto) wake ni Abul Hassan na jina lake la heshima ni Ar-Ridha.
baba yake ni Imamu Musa Al-Kadhim, na mama yake ni Bibi Umu-ul-BaninTahirah, mwanamke aliyekuwa Mchamungu sana.
KUZALIWA KWAKE
Imamu Ali Ar-Ridha (a.s.) alizaliwa mnamo tarehe 11 ya mwezi wa Dhul-Qa'adah (Mfunguo Pili) wa mwaka wa 148 Hijiriya, mjini Madina. Wakati huo baba yake Imamu Jaafar As-Sadiq (a.s.) alikuwa keshafariki mwezi mmoja uliopita, kwenye tarehe 15 ya mwezi wa Shawwal (Mfunguo Mosi) na kuzaliwa kwa mtoto huyu kulileta faraja kwa jamii hii iliyoondokewa na baba yao.
KULELEWA KWAKE
Alilelewa chini ya ulinzi wa baba yake, Imamu Mussa Al-Kadhim (a.s.) na alipitisha maisha ya miaka thelathini na mitano ya maisha haya chini ya uongozi huu wa kimapenzi na katika mazingira ya kidini hayo hayo. Ingawa katika miaka michache ya maisha yake ya mwishoni ilimbidi kutengana na mpenzi babiye wakati Imamu Musa Al-Kadhim (a.s.) ilipombidi kwenda kupambana na taabu za jela nchini Iraq, Imamu (a.s.) alikuwa tayari keshaishi na baba yake kwa muda wa miaka 28 au 29 hivi.
UIMAMUWAKE
Imamu Musa Al-Kadhim (a.s.) alielewa vizuri kuwa wafalme wa zama hizo hawatamwacha aishi kwa amani, na kuwa muda utafika mwishoni mwa maisha yake ambapo marafiki zake wapenzi hawatapata uhuru wa kuonana naye kila wapendapo kumuona, au kumjua mrithi wake baada ya kufariki kwake. Hivyo alihisi kuwa ipo haja ya kuwafanya wafuasi wa watu wa Nyumba ya Mtukufu Mtume (s.a.w.) wamfahamu vizuri mrithi wake wakati wakiwa wanaishi kwa amani mjini Madina. Hivyo aliwaita watu kumi na saba wenye cheo kutoka miongoni mwa dhuria wa Hadhrat Ali bin Abi Talib (a.s.) na Bibi Fatimah (a.s.) na 'kutangazia kuwa mrithi wake atakuwa mwanawe, Ali. Vile vile aliandika usia wake kuhusu jambo hilo na ukatiwa saini na watu sitini, wakazi wa mjini Madina.
MUDA WA UIMAMU WAKE
Imamu Ali Ar-Ridha alikuwa na umri wa miaka 35 alipofariki baba yake Imamu, Imamu Musa Kadhimu. Kazi zote na Uimamu zilimuangukia yeye, baada ya kufariki baba yake. Huu ulikuwa ni muda wa utawala wa mfalme Harun-Al-Rashid na makao yake yalikuwa Baghdad (Iraq). Wakati huu ulikuwa mgumu sana kwa dhuria wa Bibi Fatimah (a.s.). Na chini ya hali hizi mbaya, Imamu (a.s.) aliianza kazi yake ya kuitangaza dini ya kweli, na kuudumisha Ujumbe Mtakatifu.
MAISHA YAKE YA UALIMU
Nuru aliyoipewa na Mwenyezi Mungu waliyobarikiwa nayo watu wa Nyumba ya Mtukufu Mtume (s.a.w.) ilitambuliwa na marafiki zake na maadui pia. Wakati baadhi yao walipokuwa na nafasi kubwa ya kuitawanya mbegu ya elimu ya kweli, wengine walikuwa na nafasi ndogo sana ya kuwaangazia viumbe wa Mwenyezi Mungu. Baada ya Imamu Jaafar (a.s.)Imamu aliyepata nafasi kubwa ya kuutangaza Ujumbe wa Mwenyezi Mungu, alikuwa Imamu Ali Ridha (a.s.). Kabla hajaichukua kazi ya Uimamu, baba yake alikuwa akiwaelezea wanawe na watu wengine wa jamii yake kuhusu Imamu Ali Ridha (a.s.), akisema,
Ndugu yenu Ali Ridha ndiye mlinzi wa Elimu ya Watu wa Nyumba ya Mtume (s.a.w.). Mwendeeni mnapokabiliwa na matatizo ya kidini na kila mara kumbukeni asemavyo". Na baada ya kufariki baba yake, alipokuwa akiishi mjini Madina na alipokuwa na kawaida ya kukaa karibu na kaburi la Mtukufu Mtume (s.a.w.)., wanachuoni wakuu wa Fiqah walikuwa wakimjia wakimletea matatizo yao ayatatue. Bwana Muhammad bin Isa Yaqtini alihadithia kuwa wakati Amamu Ali Ridha (a.s.) alipoyakusanya matatizo yote aliyoletewa na kuyaweka katika hali ya kimaandishi idadi ya matatizo hayo ilifikia elfu kumi na nane.
MAISHAYAKE
Mfalme Harun Al-Rashid alitawala kwa muda wa miaka kumi baada ya kufariki kwake Imamu Musa Kadhim (a.s.), na kwakweli mfalme huyu wa ukoo wa Bani Abbas hakumpenda mwana huyu Mchamungu (.Imamu Ridha a.s.) zaidi ya alivyompenda yule baba Mchamungu (Imamu Kadhim). Lakini haijulikani kama mfalme huyu aliwapenda hawa Maimamu wawili kwa sababu ya kuogopa
asipoteze mapenzi yake kwa watu au labda inawezekana kwamba ilikuwa ni moyo wake tu uliomtuma kufanya hivyo; hivyo basi, mfalme Harun -Al-Rashid hakuchukua hatua yo yote ile ya kiuadui dhidi ya Imamu Ali Ridha (a.s.). Iko hadithi isemayo kwamba, siku moja mtu mmoja aitwaye Yahya bin Khalid Barmaki, ili kumvika Harun kilemba cha ukoka, alimwambia, "Sasa Ali bin Musa nae anadai kuwayu Imamu kama baba yake". Harun Al-Rashid alimjibu, "Tumemtendea mambo mengi sana baba yake: na sasa unataka niimalizie mbali jamii hiyo".
Lakini, vivyo hisia za Harun Rashid kwa watu wa Nyumba ya Mtukufu Mtume (s.a.w.) na jinsi walivyotendewa na wafalme kwa ujumla mpaka sasa yalifahamika sana kiasi cha kutomfanya yeyote yule kati ya maofisa kumheshimu Imamu (a.s.), pia wale watu miongoni mwa raia waliotaka majna yao yaandikwe katika vitabu vizuri vya serikali hawakufikiria kufanya hivyo. Watu hawakupata uhuru wa kuja kusomea Fiqah kwa Imamu (a.s) na hakupata nafasi yoyote ya kuutangazaUislamu.
Siku za mwisho za Harun Al-Rashid ziliharibiwa na maasi ya vanawe wawili. Mwanawe aitwaye Amin, aliyezaliwa kutokana la mkewe wa kwanza na aliyekuwa mjukuu wa mfalme Mansur Dawaniqi; hivyo watu wakuu miongom mwa Waarabu walimpendelea sana. Mwanawe mwingine aitwaye Mamun aliyemzaa na mjakazi wake wa Kiirani, hivyo wakuu wa baraza lake wenye asili ya Kiirani walimpendelea mtoto huyu. Maasi ya watoto hao yalimsumbua sana Harun. Alifikiria kuigawa milki yake baina ya hawa watoto wawili, hivyo alimpa Amin sehemu ya Magharibi ya milki hiyo ukiwemo mji mkuu, Baghdad, Shamu, Misr, Hijaz, na yaman. Na sehemu ya Mashariki ikiwemo Iran, Khurasan, na turkistan ilipewa Mamun, lakini kwa kweli hatua hii ingelifaulu tu kama pande zote mbili zingeliuangalia sana msingi wa "Ishi kwa amani na waache wengine waishi kwa amani".
Baada tu ya kufariki Harun hawa watoto wawili walianza kugombana wao kwa wao na baada ya kupigana kwa muda wa
miaka minne, Amin alikatwa kichwa katika mwezi wa Muharram wa mwaka 198 Hijiriya na Mamuun akawa mfalme.